Thursday 8 September 2016

MT'S THIRD BIRTHDAY

Heri ya siku yako ya kuzaliwa MT, miaka mitatu sasa duniani na naamini MUNGU atatusaidia tuendelee kuihesabu kwa mamoja na makumi tele.

Ilikuwa mara yangu ya pili kuingia "leba" na mama yako, (mara ya pili kwa mama yako pia ).... tayari tulishaandaa majina, moja la kike na moja la kiume, mama ni mama tu, alishajua kuwa utazaliwa wewe na kweli ukazaliwa wewe tukakuita Marytheresa, jina la mama mkwe wangu kipenzi na kufanya family yetu kuwa na watoto wenye majina ya mama zetu wote.
Nilikupenda kabla hata ya kutungwa kwa mimba yako, hakuna kingine zaidi ya kumpenda mtu ambaye ni kiini cha upendo wenyewe, wewe hapo mwanangu na kama waona hautoshi huu upendo niambie "niuongeze sauti". Maisha yamefanya tuwe mbali na mama yako, hatulipendi hili na tunajitahidi kulirekebisha, hii inanifanya niwe baba na mama kwako kwa wakati mmoja ili usijihisi kupungukiwa, nashukuru MUNGU angalau hili linamudika japo ukweli ni kuwa bado tunamuhitaji sana mama yako, tusamehe mwanangu ila fahamu uko salama nami, mama yako kuniamini kiasi cha kuniacha nawe kunadhihirisha "usalimini".
Wewe ni nguvu na uwezo wangu, sikujua kwamba mimi ni Mwanasaikolojia, Daktari, Bingwa wa mahesabu na vingine vingi mpaka pale nilipoongeza ukaribu ktk kukulea, ukaribu unaonifanya kuwa sehemu kuu ya maisha yako, ukaribu wa si tu kutoa hela ya chakula bali kukupikia na kukulisha kwa mikono yangu, ukaribu wa kujua muda gani na mara ngapi nikuamshe usiku ili usikiloweshe kitanda, ukaribu wa kujua cheko lako lipi ni la furaha yako kuu.
Babaako nimekuwa sio mzuri sana when it comes to ahadi, nimewaangusha baadhi ya watu nikiwamo mimi mwenyewe, wajua nabaki kuwa binadamu kama binadamu wengine...lakini sitaki hii iwe excuse, NAKUAHIDI na wala siogopi kukuahidi kutimiza ahadi zote nilizojiahidi mimi na mama yako kuhusu wewe, MUNGU na atusaidie sana.
Nafurahi unajua vitu vingi kabla hata hujaanza shule, nitambue mchango wa dadaako KITA kwa uwezo ulionao, amekuwa mwalimu mzuri kwako, good news ni kwamba Vile vilio vyako vya kutaka kuongozana na Kita kwenda shule kila asuhuhi apandapo gari, leo vinafikia kikomo....Hii najua ndio zawadi utakayoipenda sana, kwamba kuanzia

JUMATATU UTAVAA UNIFORM KWENDA SHULE NA KITA
Wynjones Kinye
August 12 at 10:14am