Wednesday 7 September 2016

KITA'S SECOND BIRTHDAY

Kita at two
umezaliwa tena 'KITAWETU' na hii ni barua ya pili kwako.
Mwaka jana tar ya leo nilikueleza mengi ikiwa ni pamoja furaha uliyoipanda kwenye mioyo yetu! Mwaka huu nafurahi zaidi na kifua kikiwa mbele nafurahi kukuambia kwamba tayari mimi na mama yako Agatha Nicholaus tu mume na mke hivyo wewe na sisi ni familia iliyo kamili sasa na yevye baraka na vibali vyote toka kwa Mungu na Wazazi.


Bado tuna ndoto kubwa kwako, nyingine binafsi sijui zitatimiaje lakini zitatimia tu kwa sababu tunaishi.
Bado wewe ni pambo la nyumba yetu na mioyo yetu, wazipa tabasamu nyuso zetu hata pale maisha yanapotupiga, kwa ajili yako tunasimama na kusonga mbele.
Bado watupa thamani kama wazazi, bado watupa ujasiri, bado watutia nguvu ya kusema hili na hili tutalifanya.
Najua bado sijawa baba ambaye mimi mwenyewe nataka niwe kwako, hii inaniumiza lakini kuwa mvumilivu mwanangu...kule upareni twasema "gumirija vyedi vyedhie" yaani vumilia vizuri vyaja, nilishaahidi kuwa hutaishi maisha niliyoishi mimi, hutasoma shule nilizosoma mimi, hutapambana na daladala ama kutembea umbali mrefu kwenda shule.
KITA! Una booonge la mama, najua u mdogo lakini unaenjoy upendo wake kwako, zaidi unaona ama kuhisi namna anavyojitoa kwa familia, ni bahati kubwa kuwa naye kama MKE na kuwa nawe kama MTOTO, kua uendelee kuliona hili ili ujifunze ayafanyayo hata uyafanye muda wako ukiwadia.
Upendo mwingi umekuzunguka Kita! Ndugu, Marafiki, Majirani na kila mtu amekuongelea vizuri...hili linatosha kukupa ulinzi wa furaha, naamini upendo huu utaendelea kukuzunguka kadri uongezavyo miaka, usiharibu hapo katikati, sawa mama?
Nina mengi ya kusema Kita, hata nikipewa siku nzima sitayamaliza hapa...nifupishe tu kwa kusema NAKUPENDA SANA, NAKUJALI SANA, na NAOTA MENGI KUKUHUSU.
Baba.