Wednesday 7 September 2016

MT'S FIRST BIRTHDAY

Happy Birthday Baby MT....ya kwanza hii mwanangu na veeeerrrrrry maalum, niseme nini babaako zaidi ya kumshukuru Mungu aliye juu kwa zawadi hii ya ghali mno?!! Hivi wajua navyojisikia kushuhudia ukuaji wako siku baada ya siku...? Kwakweli ni zaidi ya kumilikishwa dunia, ni nusu ya kuwa peponi.

Nilikuwa pale wakati shujaa mamaako akikuleta duniani (nani kama mama?)...nililia alipolia kwa maumivu, ulipotoka tu na kulia kwa mara ya kwanza mimi na yeye tukalia zaidi huku tukitabasamu...kilo 3.7 alizitoa kijasiri. Unajua sauti yako baada ya kulia ilizungumza maneno mengi sana?!! Sauti ile ilimaanisha vingi sana kwetu (nitakuambia siku moja), mimi na mamaako tulitazamana tukiwa tumeshikana mikono kwa nguvu sana tukasali kumshukuru na kumsifu Mungu kwa zawadi wewe...tulikwisha kuandalia jina mwaya...tukaanza kujulisha watu kuwa Marytheresa kazaliwa.
Umeongeza baraka kwenye nyumba yetu, umekoleza utamu kwenye ndoa yetu, umempa heshima ya cheo Kita...eti naye ni dada!! Anajidai sana na tunawaangalia na kufurahi sana kila siku. Natamani kuwaona mkikua pamoja mngali na upendo mlio nao kwa kila mmoja, sisi tunajitahidi na tutajitahidi kuwatengenezea maisha mazuri, si yale sisi wazazi wenu tuliyopitia...hayakuwa mabaya lakini kuna viwili vitatu hatutopenda mviexperience.
Nakuombea kwa Mungu ukue salama ukiwa mwenye afya tele, kwanini tusimshukuru Mungu ikiwa gonjwa kubwa lililowahi kukupata wewe ni mafua na kikohozi?? Sifa na Utukufu kwako ee Yesu. Nazidi kukuombea mwaka huu wa kwanza kuwa mwanzo wa safari yako ya uzeeni, ufike kule ukiwa mwenye busara na vingi vya kutoa kwa watu wenye uhitaji na wasio na uhitaji, uwe majibu ya maswali yaliyoshindikana duniani huku ukitembea katika njia inayompendeza Mungu baba yetu.
TUNAKUPENDA MT, ISHI MINGI.
Dad.