Wednesday 7 September 2016

MT'S SECOND BIRTHDAY

Heshima na utukufu kwako ee Mungu kwa kutukuzia zawadi hii yako kwetu, malaika wetu...furaha yetu...sababu yetu ya kuimarika...binti yetu MT...it's her 2nd birthday (ona siku zinavyokimbia).
Dear MT

mimi na mama yako tulimuomba Mungu wewe akatupatia wewe...wewe ni jibu la maombi yetu na kila siku tunayojaaliwa kuiona ni ya kumshukuru Mungu kwa wewe...kwa moyo wa dhahabu kama wa dada yako niseme kuwa umekuwa "mwenza" mzuri sana wa Kita, naona jinsi mnavyouimarisha umoja wenu kila siku nasi tunajivunia sana.
Kama baba unanihamasisha sana kupigana, sijui nimeshinda mapambano mangapi kwa ajili yako...ni mengi na kamwe sitohesabu kwani ni jukumu langu kwako, kitokacho kwangu si kitu zaidi ya kiingiacho kwako....akili na nguvu zangu ni kwa ajili ya furaha na mahitaji yako...of course na moyo na roho yangu ni kwa kukupenda na kukufurahia.
Kwa miaka miwili hii tayari umeshaonyesha dalili zoote nzuri za kuwa mtoto mwema kwetu na mtu mwema kwako wewe mwenyewe...kama mzazi nitahakikisha hubadiliki...usikivu wako kama mtoto endelea nao siku zote za maisha yako...ni kutoka usikivuni utavumbua na kugundua visivyoonwa....upendo wako kwetu na kwa wanaokuzunguka pia endelea nao, naona pia unavojipenda wewe mwenyewe (muhimu sana mwanangu)...ila unanivutia unavyojipenda pasipo kujipendelea...najivunia vitu hivi na vingine vingi ulivyonavyo ndani yako...vinaongeza sana thamani yako kama binadamu, leo nakuambia hivi ni salaha muhimu kwako kuyakabili maisha zaidi ya uzuri ulionao (wewe ni mzuri sana mwanangu).
Umemaliza mwaka wako wa kwanza na sindano...malaria imekutesa kweli...umepungua kilo kadhaa, cha kumshukuru Mungu ni kuwa unauanza mwaka mpya ukiwa na afya...tabasamu lako asubuhi ya leo baada ya kukupa busu la birthday ni uthibitisho mkubwa...na hata uliponikumbatia nikahisi joto lako kuwa normal tofauti na jana na juzi....tunamshukuru Mungu na ufundi wa daktari ktk kupigania afya yako.
Mwakani nawe utaanza shule, uko tayari kabisa mwanangu...naona jinsi nawe unavyoshughulika pindi Kita afanyapo assignments zake, jinsi unavyorudia numbers..sounds...na alphabets anazoimba...hata siku ulipoingia darasani kwa Kita ulifurahi kwa namna ya kipekee...kwa furaha nilifuta "kachozi"
Siwezi weka nukta pasipo kumshukuru mamaako Agatha Nicholaus kwa ajili yako...kwa ajili yenu...kwa ajili yangu...kwa ajili yetu. Amekuwa muhimili mkubwa na muhimu sana wa familia yetu, tumpende kumtia nguvu zaidi...tumuheshimu na kumlinda asikate tamaa....nyie ni nguvu yangu...nawapenda sana.
HAPPY BIRTHDAY MT